Psalms 29:3-9

3 aSauti ya Bwana iko juu ya maji;
Mungu wa utukufu hupiga radi,
Bwana hupiga radi juu ya maji makuu.

4 bSauti ya Bwana ina nguvu;
sauti ya Bwana ni tukufu.
5 cSauti ya Bwana huvunja mierezi;
Bwana huvunja vipande vipande
mierezi ya Lebanoni.
6 dHufanya Lebanoni irukaruke kama ndama,
Sirioni
Yaani Mlima Hermoni.
urukaruke kama mwana nyati.
7 fSauti ya Bwana hupiga kwa miali
ya umeme wa radi.
8 gSauti ya Bwana hutikisa jangwa;
Bwana hutikisa Jangwa la Kadeshi.
9 hSauti ya Bwana huzalisha ayala,
na huuacha msitu wazi.
Hekaluni mwake wote wasema,
“Utukufu!”
Copyright information for SwhNEN